Thursday 14 January 2016

URA Mabingwa Wapya Mapinduzi Cup

URA Mabingwa Wapya Mapinduzi Cup

Tarehe January 14, 2016
Kikosi cha mabingwa wa michuano ya mapinduzi Timu ya URA kutoka Uganda
Kikosi cha mabingwa wa michuano ya mapinduzi Timu ya URA kutoka Uganda
Timu ya URA kutoka Uganda imeibuka na ubingwa wa kombe la mapinduzi katika fainali iliyomalizika mapema jana kwa kuitandika Mtibwa Sugar jumla ya mabao 3-1.
Mtibwa wanaandika histori nyingine ya kulikosa kombe hilo kwa mara ya pili mfululizo ambapo mwaka jana waliingia fainali na Simba na kulipoteza kombe hilo .
Bao la kwanza lililofungwa na Julius Ntambi kwa kichwa, lilidumu hadi mwisho wa dakika 45 na timu ziliporejea uwanjani ilionekana kama Mtibwa Sugar wamejiandaa kusawazisha
Hata hivyo, mambo hayakuwa mazuri baada ya kufungwa mabao mengine harakaharaka yakifungwa na David Lwasa aliyeingia kipindi cha pili ambaye alitumia makosa mara mbili ya mabeki wa Mtibwa Sugar ambao mwishoni walionekana kuchoka.
Bao pekee la Mtibwa Sugar lilifungwa dakika ya 90 na Jaffar Salum baada ya kipa wa URA kufanya mzaha na mfungaji akampokonya mpira na kuutupia wavuni.

clouds stream