Sunday 10 January 2016

Madereva Mwendokasi Waagoma Kisa Mshahara

Madereva Mwendokasi Waagoma Kisa Mshahara

Tarehe January 11, 2016
Mradi wa mabasi yaendayo kasi.
Mradi wa mabasi yaendayo kasi.
Mradi wa mabasi yaendayo kwa kasi uliopangwa kuanza kazi leo na kusitishwa kutokana na kutokamilika kwa pendekezo la nauli,madereva wake wamegoma kufuatia uongozi wa mabasi hayo kuwapa mkataba wa kazi usiokidhi mahitaji.
Kwa mujibu wa madereva hao wamesema kwamba wamegoma kutokana na kupewa mkataba wenye mshahara mdogo ambao ni shilingi shilingi laki 4  huku makubaliano ya awali ya shilingi laki 8.
Madereva hao wamesema pia wameshangazwa na kitendo cha uongozi wa mabasi hayo kuwapa mkataba wa kazi bila ya kuwapatia nakala yake jambo ambalo wamesema ni kinyume cha taratibu za ajira.
Mgomo huo umetokea kituo kikuu cha mabasi yaendayo haraka kilichopo eneo la Kamata jijini Dar es salaam.

clouds stream