Thursday 28 January 2016

Magufuli Amteua Banzi Naibu Gavana Benki Kuu

Magufuli Amteua Banzi Naibu Gavana Benki Kuu

Tarehe January 28, 2016
Rais Dkt.John Pombe Magufuli.
Rais Dkt.John Pombe Magufuli.
Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, amemteua Ndugu Julian Banzi Raphael, kuwa Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imebainisha kuwa kabla ya uteuzi huu Ndugu Julian Banzi Raphael alikuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Biashara na Viwanda, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Ndugu Julian Banzi Raphael anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Ndugu Juma Reli ambaye muda wake umemalizika tarehe 12 Julai, 2015.

clouds stream