Thursday 17 August 2017

Bi Mugabe aomba kinga ya kidiplomasia dhidi ya kesi

Mugabe na mkewe

Mugabe na mkewe
IMG-20170426-WA0006

Serikali ya Zimbabwe imemuombea mkewe Mugabe kinga ya kidiplomasia dhidi ya kesi ya ushambuliaji inayomkabili nchini Afrika kusini , maafisa wa polisi wa taifa hilo wamesema.

''Grace Mugabe alikuwa bado yupo Afrika Kusini'' iliongezea wakipinga ripoti za awali kwamba alikuwa amerudi nchini Zimbabwe.

Mwanamitindo mwenye umri wa miaka 20 amemtuhumu bi Mugabe kwa kumshambulia katika hoteli moja mjini Johannesburg.

Polisi walitarajia kwamba bi Mugabe angejiwasilisha kwao mwenyewe siku ya Jumanne lakini hakufanya hivyo.

''Serikali ya Zimbabwe imewasilisha ombi la kumlinda kidiplomasia'', wizara hiyo ilisema katika taarafa yake.

clouds stream