Friday 11 August 2017

Tume ya uchaguzi Kenya yashangazwa na matokeo ya upinzani

Image result for kenya

IMG-20170426-WA0006

Tume ya Uchaguzi ya Kenya imesema ni mapema na ni kinyume cha sheria kwa mgombea wa upinzani Raila Odinga kujitangazia kuwa ameshinda uchaguzi wa Kenya.

Alhamisi, muungano wa upinzani wa NASA ulichapisha matokeo ambayo yanaonyesha kuwa Raila Odinga amemshinda Rais wa sasa Uhuru Kenyatta, ambapo pia waliitaka tume ya uchaguzi imtangaze Odinga kuwa ndiye Rais mteule.

Hata hivyo matokeo ya awali hadi sasa yaliyotangazwa na tume hiyo yanaonyesha Rais wa sasa Uhuru Kenyatta bado anaongoza dhidi ya mpinzani wake Raila Odinga.

Mwandishi wetu Anne Soy alifanya mahojiano na Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati.

Kwanza alimuuliza, je tume hiyo imepokea barua yoyote kutoka kutoka upinzani?

clouds stream