Thursday 31 August 2017

Bodi Ya Mikopo Yaongeza Muda Wa Kuomba Mikopo.

008.CHUO_-620x308
IMG-20170426-WA0006
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imeongeza muda wa maombi ya kuomba mkopo kwa wanafunzi wa mwaka wa masomo wa 2017/2018.
Kwa mujibu wa mabadiliko hayo, wanafunzi wa elimu ya juu sasa wataweza kuomba mkopo hadi kufikia Septemba 11, ikiwa ni siku saba mbele ya iliyokuwa tarehe ya mwisho hapo awali ya Septemba 4, mwaka huu.
Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru amesema hadi kufikia jana, jumla ya waombaji 49, 282 wamekwishaingiza taarifa zao katika mtandao wa HESLB kwa ajili ya kuomba mkopo.

clouds stream