Friday 4 August 2017

Neymar: Paris St-Germain wamnunua nyota wa Barcelona kwa rekodi ya dunia ya euro 222m

Neymar

Neymar alishinda vikombe tisa misimu minne aliyokaa Barcelona

IMG-20170426-WA0006

Paris St-Germain wamekamilisha kumnunua mshambuliaji wa Brazil, Neymar, kwa ada iliyoweka rekodi mpya ya ununuzi wa mchezaji ya euro 222m (£200m) kutoka Barcelona.

Ununuzi huo wa mchezaji huyo wa miaka 25 umevunja rekodi ya awali iliyowekwa Paul Pogba aliporejea Manchester United kutoka Juventus kwa £89m Agosti 2016.

Atakuwa analipwa euro 45m (£40.7m) kwa mwaka - euro 865,000 (£782,000) kila wiki - kabla ya kutozwa ushuru katika mkataba wake wa kwanza wa miaka mitano. Hiyo ni jumla ya £400m.

Neymar amesema amejiunga na "mojawapo ya klabu zenye ndoto kuu zaidi Ulaya".

"Ndoto kuu ya Paris St-Germain ilinivutia kujiunga na klabu hiyo, pamoja na kujitoleza kwao na nguvu zinazotokana na hili," amesema.

"Najihisi niko tayari kuanza kazi. Kuanzia leo, nitafanya kila niwezalo kuwasaidia wachezaji wenzangu wapya."

Klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Ufaransa imepanga kuwa na kikao na wanahabari mwendo wa saa 12:30 BST Ijumaa (saa nane unusu Afrika Mashariki).

Neymar baadaye atatambulishwa rasmi kwa mashabiki wa PSG Jumamosi wakati wa mechi yao ya kwanza kabisa ya msimu mpya, ambayo itakuwa nyumbani uwanja wa Parc des Princes dhidi ya Amiens.

Neymar with Lionel Messi and Luis Suarez after the Copa del Rey final
Neymar akiwa na Lionel Messi na Luis Suarez na watoto wao baada ya kushinda Copa del Rey

Neymar alikuwa amefika kituo cha mazooezi cha Barcelona Jumatano akiandamana na babake na mwakilishi wake na kufahamisha klabu hiyo ya Uhispania kwamba angetaka kuondoka.

Alipewa ruhusa na meneja wa Barca Ernesto Valverde kwenda "kupanga mustakabali wake".

Nchini Uhispania, kifungu cha kumwachilia mchezaji kutoka kwa mkataba wake kinaweza tu kufunguliwa kwa mchezaji kulipa pesa yeye binafsi.

Neymar alipofika na pesa Alhamisi kulipa hata hivyo, maafisa wa La Liga walikataa malipo hayo.

Kulitokea majibizano kati ya maafisa wa La Liga na wasimamizi wa Ligue 1.

La Liga wanaamini PSG huenda wanakiuka sheria za uchezaji haki kifedha (FFP) kwa kumnunua mchezaji huyo wa Brazil.

Baada ya kushindwa kulipa pesa hizo kwa La Liga, wawakilishi wa Neymar walilipa euro 222m (£200m) katika afisi za Barca badala yake.

Neymar alijiunga na Barca mwaka 2013 na akashinda mataji mawili ya La Liga na moja la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

PSG wameorodheshwa wa 11 kwa thamani duniani na Forbes lakini ni mara yao ya kwanza kwao kuvunja rekodi ya dunia katika kumnunua mchezaji.

Neymar ni nani?

  • Alizaliwa Mogi das Cruzes, viungani mwa Sao Paulo, 5 Februari 1992

  • Alianza uchezaji wake Santos kwa kutia saini mkataba wa kulipwa Januari 2009

  • Amesalia kuwa mfungaji mabao mengi zaidi Santos baada ya enzi ya Pele ambapo aliwafungia mabao138 mechi 229.

  • Alihusishwa na kuhamia Real Madrid, Chelsea na Manchester United kabla ya kuchukuliwa na Barcelona Juni 2013 akiwa na miaka 21.

  • Alichezea Barca mechi yake ya kwanza dhidi ya Levante Agosti 2013 na akawafungia mabao 105 na kusaidia ufungaji wa mengine 80 katika mechi 186 alizochezea klabu hiyo ya Catalona.

  • Alichezea timu ya taifa mara ya kwanza akiwa na miaka18 na amefunga mabao 52 katika mechi 77 alizochezea Brazil

Neymar akiwa Barca msimu uliopita
MechiDakika alizochezaMabaoDakika kwa kila goliKusaidia ufungaji
453,9722019927

Neymar
Neymaralifunga bao la kasi zaidi historia ya Olimpiki sekunde 14 pekee baada yamechi ya nusufainali dhidi ya Honduras kuanza Olimpiki Rio 2016

Pogba (£89m) Bale (£85m) Ronaldo (£80m) Higuain (£75m) Lukaku (£75m) Suarez (£75m) Rodriguez (£63m) di Maria (£60m) de Bruyne (£55m) Zidane (£46m)
Image captionThe top 10 most expensive deals (fees as reported in sterling at the time) before Neymar

Neymar's £198m transfer fee in context


clouds stream