Korea Kaskazini ilifanya majaribio ya makombora manne

China imependekeza kwamba Korea Kaskazini ipige marufuku majaribio yake ya makombora pamoja na teknolojia yake ya nyuklia ili kuzima wasiwasi unaoendelea.
Waziri wa maswala ya kigeni Wang Yi alisema kuwa kwa makubaliano hayo Marekani na Korea Kusini zitasitisha mazoezi ya kijeshi ya pamoja ambayo yanakasirisha Korea Kaskazini.
Ombi hilo linajiri baada Korea Kaskazini kufanyia majaribio makombora yake manne siku ya Jumatatu na kukiuka vikwazo vya kimataifa.
Ili kujibu hatua hiyo, Marekani imeanza kuweka mfumo wa kujilinda dhidi ya makombora nchini Korea Kusini.
