Monday 27 March 2017

Wasichana waliovalia suruali za kubana wazuiwa kuabiri ndege ya United Airlines Marekani

Ndege za United Airlines

Shirika hilo la ndege limeshutumiwa sana kwenye Twitter
img-20161130-wa0008

Shirika la ndege la United Airlines nchini Marekani limeshutumiwa sana baada ya kudaiwa kuwazuiwa wasichana wawili waliokuwa wamevalia suruali ndefu za kubana kuabiri ndege hiyo.

Kisa hicho kilitokea kwenye safari ya ndege iliyokuwa ikitokea Denver kuelekea Minneapolis Jumapili asubuhi, mwanaharakati Shannon Watts amesema.

Shirika la United limesema wasichana hao walikuwa wanasafiria hati maalum, ambayo hutumiwa na wafanyakazi wa shirika la ndege na wageni wao.

United wamesema huwa kuna kanuni za mavazi kwa wanaotumia hati hiyo kusafiria.

Shirika hilo limefafanua kwamba abiria wa kawaida, ambao wanalipia tiketi zao, wako huru kuvalia mavazi yao ya kubana.

Hati hiyo maalum ya kusafiria ya United huwawezesha walio na hati hiyo kusafiri kwa ndege bila malipo au kwa tiketi za bei nafuu sana.

Kanuni za mavazi kwa wanaotumia hati hiyo huel

clouds stream