Saturday 11 March 2017

Donald Trump amwalika rais wa Palestina Mohamud Abbas

Rais wa Palestina Mohamud Abbas

Rais wa Palestina Mohamud Abbas
img-20161130-wa0008

Ikulu ya white house inasema kwamba rais Donald Trump amemwalika kiongozi wa Palestina, Mohamud Abbas, nchini Marekani hivi karibuni.

Bwana Trump amemwalika Abbas baada ya mazungumzo ya kwanza ya simu na kiongozi huyo tangu aingie maamlakani.

Trump amependekeza kuhusika katika juhudi za amani mashariki ya kati, japo viongozi wa Palestina wanalalamika kwamba sera ya kigeni ya rais Trump inaonekana kupendelea Israeli.

Hakujakuwa na mazungumzo ya amani ya haja kati ya Israel na Palestina tangu mazungumzo ya amani yalioanzishwa na Marekani kugonga mwamba mnamo mwezi Aprili 2014.

Msemaji wa Trump Sean Spicer alithibitisha siku ya Ijumaa kwamba rais wa Marekani alimualika Abbas katika ikulu ya Whitehouse hivi karibuni.

Rais Donald Trump wa Marekani na waziri mkuu Benjamin Netayahu wa Israel
Rais Donald Trump wa Marekani na waziri mkuu Benjamin Netayahu wa Israel

Rais huyo alimwambia kiongozi huyo wa Palestina kwamba watajadiliana vile watakavyoanzisha tena mazungumzo ya amani kulingana na msemaji wa Abbas aliyenukuliwa na Reuters akisema.

Alisema kwamba bwana Trump alisisitiza kuhusu juhudi zake za mpango wa amani ambao utaleta amani ya kweli kati ya Palestina na Israel.

Maafisa wa Palestina walikuwa wamesema kwamba kabla ya simu hiyo ya siku ya Ijumaa. bwana Abbas atamsisitizia rais huyo wa Marekani kuhusu ujenzi wa majumba ya walowezi katika ardhi ya Palestina na umuhimu wa mataifa mawili yalio huru.

clouds stream