Thursday 16 March 2017

UN yaitaja Israel kama nchi ya kibaguzi

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu
img-20161130-wa0008

Umoja wa mataifa umetoa ripoti inayoituhumu Israel kuwa ni nchi ya kibaguzi, madai ambayo nchi hiyo pamoja na washirika wake wameyakana kwa nguvu.

Ripoti hiyo inasema kuwa Israel imeanzisha mfumo unaowatenga raia wa kutoka Palestina.

Imetolewa na kamisheni ya uchumi na masuala ya kijamii kwa nchi za Magharibi mwa bara la Asia ambapo mkuu wake Rima Khalaf amesema kuwa hii ni kwa mara ya kwanza UN kukiri kuwa Israel ni nchi ya kibaguzi.

Lakini umoja wa mataifa umesema kuwa ripoti hiyo inawakilisha tu mawazo ya waandishi walioiandika ambao ni kutoka Marekani.

Israel katika taarifa yake imesema ni nchi yenye demokrasi zaidi katika nchi za Mashariki ya kati.

clouds stream