Sunday 19 March 2017

Nyota wa Rock and roll Chuck Berry amefariki

Charles

Charles "Chuck" Berry alizaliwa huko St Louis, Missouri mnamo Tarehe 18 Octoba 1926
img-20161130-wa0008

Mmoja wa waanzilishi wa muziki aina ya rock and roll, Chuck Berry, amefariki akiwa na umri wa miaka 90 nyumbani kwake katika jimbo la Missouri, huko Marekani.

Muimbaji na mchezaji gitaa huyo alifahamika kote duniani kwa vibao vikali alivyovizindua miaka ya 50s, ukiwemo kibao "Roll Over Beethoven", ''Sweet Little Sixteen'' na "Johnny B. Goode".

Alianzisha utumiaji wa gitaa wa mchezaji mmoja maarufu kama solos na showmanship kwa wapenzi wa mziki na kuhamasisha mabendi kama vile The Beatles na the Rolling Stones.

Risala za rambi rambi zimekuwa zikimiminika kutoka kwa wanamziki wenzake.

Berry, pichani mwaka 1965, alizindua kibao chake cha kwanza miaka ya 50s
Berry, pichani mwaka 1965, alizindua kibao chake cha kwanza miaka ya 50s

Bruce Springsteen anasema kuwa, Berry alikuwa mtunzi hodari mno wa magoma aina ya rock `n' roll kuwahi kuishi duniani.

Mick Jagger wa Rolling Stones naye anasema kwamba, 'aliasha moto wa miaka ya ujanani na kuingiza uhai kwenye ndoto yetu".

Miezi kadhaa iliyopita, wakati wa maadhimish

clouds stream