Charles "Chuck" Berry alizaliwa huko St Louis, Missouri mnamo Tarehe 18 Octoba 1926

Mmoja wa waanzilishi wa muziki aina ya rock and roll, Chuck Berry, amefariki akiwa na umri wa miaka 90 nyumbani kwake katika jimbo la Missouri, huko Marekani.
Muimbaji na mchezaji gitaa huyo alifahamika kote duniani kwa vibao vikali alivyovizindua miaka ya 50s, ukiwemo kibao "Roll Over Beethoven", ''Sweet Little Sixteen'' na "Johnny B. Goode".
Alianzisha utumiaji wa gitaa wa mchezaji mmoja maarufu kama solos na showmanship kwa wapenzi wa mziki na kuhamasisha mabendi kama vile The Beatles na the Rolling Stones.
Risala za rambi rambi zimekuwa zikimiminika kutoka kwa wanamziki wenzake.
