Tuesday 29 November 2016

Frederick Sumaye anyang'anywa ardhi

Tanzania

Waziri mkuu mstaafu wa Tanzania katika awamu ya tatu Fredrick Sumaye

Rais wa Jamhuri ya Tanzania amefuta hati ya umili ardhi ya shamba kubwa lililokuwa likimilikiwa na waziri mkuu mstaafu Frederick Sumaye kwasababu zilizoelezwa na serikali wa mtaa kuwa liliachwa bila kuendelezwa .

Hatua hiyo imekuja baada ya Tanzania kuzindua kampeni kubwa ya kurejesha ardhi mikononi mwa watanzania ambayo haijaendelezwa na wawekezaji waliomilikishwa awali na kuwapa wakulima masikini .

Hata hivyo, Frederick Sumaye ambaye aliwahi kuwa waziri mkuu kwa muda wa miaka kumi kuanzia mwaka 1995 na kuamua kuhamia kambi ya upinzani baada ya uchaguzi wa Tanzania mwaka wa jana uamuzi ulioelezwa kuwa na msukumo wa kisiasa.

Sumaye alisema kama lengo la kumnyang'anya ardhi yake ni jaribio la kumlazimisha kurejea katika chama tawala, "wasahau ''.

clouds stream