Sunday 20 November 2016

WENGER, MOURINHO BADO HAKIJAELEWEKA, HIVI NDIVYO WALIVYOPEANA MKONO BAADA YA GAME

Unaweza kusema hawa wazee wana lao jambo. Jose Mourinho na Arsene Wenger wanaonekana kweli hawaivi chungu kimoja.

Baada ya mechi ya Ligi Kuu England kati ya Manchester United dhidi ya Arsenal, makocha hao walipeana mkono kwa staili ambayo inaonyesha ilimradi.

Mara baada ya mechi walikutana na kupeana mkono kama sehemu ya kutimiza wajibu lakini hakuna aliyemtazama mwenzake usoni wala kuzungumza.

 
Mechi hiyo iliisha kwa sare ya bao 1-1, Arsenal wakisawazisha mwishoni kupitia Mfaransa Olvier Giroud aliyeingia kipindi cha pili.




clouds stream