Thursday 16 February 2017

Diamond Platinumz Afafanua Sababu Za Kuitwa Na Kuripoti Polisi

C4tzofVWYAAtjVT
img-20161130-wa0008

Msanii, Diamond Platinumz amefafanua sababu za yeye kuripoti katika kituo cha polisi na kusema kuwa ilikuwa ni kwasababu ya uendeshaji mbaya wa gari huku kukiwa na picha zilizosambaa katika mitandao ya kijamii zikimuonesha yupo kituo cha polisi.

Diamond amethibitisha hilo kupitia Instagram yake kwa kuandika >> ‘picha hizo leo nilireport kituo kikuu cha polisi wa usalama barabarani kutokana na video clip tuliyopost naendesha gari barabarani bila kufunga mkanda na pia kuachia usukani na  kucheza‘

‘Nikapewa Onyo na kulipa faini kwa mujibu wa sheria… tafadhali watanzania na Vijana wenzangu… tuhakikishe tunafunga mikanda pindi tupandapo na tuendeshapo Magari Maana ni Hatari kwa Maisha yetu na inaweza kukupeleka kunyea debe.

 Kwa mujibu wa Diamond, amepewa onyo na kulipa faini kutokana na kosa hilo. Kamanda wa Polisi Usalama Barabarani, Kamanda Mpinga alimuita msanii huyo kituo cha polisi baada ya kuona ‘clip’ hiyo.

Katika kipande hicho cha video, Diamond anaonekana akiwa na mpenzi wake Zari, mama yake pamoja na watoto ndani ya gari linaloendeshwa na Diamond wakisikiliza na kucheza nyimbo mpya ya Msanii huyo ya “Marry Me” aliomshirikisha staa wa Marekani, Neyo, na ndipo Platinumz anaachia usukani na kuungana na Zari katika kuserebuka mziki.

clouds stream