Thursday 9 February 2017

Mkuu Wa Wilaya Shinyanga Afuata Nyayo Za Makonda Anasa Watu


Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na Waanndishi wa Habari ofisini kwake.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na Waanndishi wa Habari ofisini kwake leo.
img-20161130-wa0008

Sakata la Madawa ya Kulevya limeanza kutikisa kwa kasi mkoani Shinyanga ambapo watu 17 wamekamatwa wakituhumiwa kutumia madawa ya Kulevya pamoja na Mirungi.

Kwa mujibu wa mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro wakati anazungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake leo amesema ofisi yake imepokea majina ya watu 20 wanaojihusisha na masuala ya madawa ya kulevya.

Amesema hadi sasa watu 17 wanashikiliwa na Polisi, ikiwa ni kutii agizo la Rais Dkt. John Magufuli aliyetaka Vita dhidi ya Dawa za Kulevya ienee nchi nzima.

Amesema baada ya kupata majina kutoka kwa wananchi kuwa watu hao wanajihusisha na masuala ya madawa ya kulevya sasa kimeundwa kikosi kazi cha kufuatilia ukweli kuhusu watu hao.

Mkuu huyo wa Wilaya amesisitiza kuwa watumiaji na wauzaji wa madawa ya kulevya hawapo Dar pekee wapo nchi nzima hivyo wanaendelea na msako kila kona ya mtaa ili kuhakikisha kuwa madawa ya kulevya yanakomeshwa mkoani humo.

clouds stream