Friday 17 February 2017

TFF Yaonya Mabango Ya Kashfa Yanga Ikiwakaribisha Wacomoro

YANGA-1
img-20161130-wa0008

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limeonya mashabiki wa mpira wa miguu nchini kutokuingia uwanjani na mabango ya aina yoyote yenye ujumbe wa kuikashifu Serikali au uongozi wa Shirikisho hilo.

Onyo hilo limetolewa leo ikiwa ni siku moja kabla ya mchezo wa Kimataifa wa Klabu Bingwa Afrika kati ya wenyeji Yanga na Ngaya ya Comoro.

TFF imesema kuwa litawatia nguvuni kwa mujibu wa sheria na taratibu mashabiki watakaoikashifu serikali ama uongozi wa shirikisho hilo kwa kuingia na mabango uwanjani yenye jumbe tofauti hapo kesho katika mchezo wa kimataifa wa klabu bingwa Afrika kati ya wenyeji, Yanga dhidi ya Ngaya ya Nchini Comoro.

clouds stream