Thursday 9 February 2017

UPDATE: Manji Azuiwa Asiondoke,Arudishwa Kituo Cha Polisi Gwajima Akiwasili Kituoni


Manji akizuiwa na askari polisi kutoka nje ya kituo cha polisi.
Manji akizuiwa na askari polisi kutoka nje ya kituo cha polisi.
img-20161130-wa0008

Kutoka Central Police Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Yanga na Mfanyabiashara, Yusuph Manji amezuiwa kutoka kituoni hapo baada ya kufanyika mahojiano.

Polisi wameagizwa wamzuie asiondoke na amerudishwa kituoni hapo huku ikidaiwa kuwa ni kwa ajili ya kumsubiri Kamanda Simon Sirro.

Wakati huohuo, Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima anadaiwa kuwasili kituoni hapo kuonana na Kamanda Simon Sirro.

Mchungaji Gwajima amewasili kituo cha polisi majira ya saa 7:30 mchana akiwa ameongoza na wafuasi wake, kutii agizo la Mkuu wa Mkoa Paul Makonda,ambaye watuhumiwa wote 65 aliowataja jana katika sakata la dawa za kulevya, aliwataka kufika kesho Ijumaa saa 5 asabuhi kituo cha Polisi kati kwa mahojiano zaidi.Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Mchungaji Gwajima akionekana kufurahia jambo wakati akiwasili kituo cha polisi kati majira ya saa 7:30 mchana akiwa ameongoza na wafuasi wake.

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Mchungaji Gwajima akionekana kufurahia jambo wakati akiwasili kituo cha polisi kati majira ya saa 7:30 mchana akiwa ameongoza na wafuasi wake.

clouds stream