Thursday 9 February 2017

Rais Kenyatta Azua Gumzo Kusakata Muziki Ikulu


Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta akisakata Muziki Ikulu.img-20161130-wa0008

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta (Katikati) akisakata Muziki Ikulu. Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amezua gumzo kufuatia kucheza muziki alipokutana na kundi moja la wachezaji densi ndani ya mjengo wa Ikulu ya Nairobi siku ya Jumatano.

Kwenye mitandao ya kijamii Watu wamekuwa wakitumia #DabOfShame, kumkosoa rais huyo, wakisema analenga tu kuimarisha kampeini yake, ilihali taifa hilo liko katika lindi la matatizo chungu nzima, ikiwemo mgomo wa muda mrefu wa madaktari na wahudumu wa matibabu.

Hivi karibuni Rais Kenyatta amekuwa akikutana na watu mashuhuri na wasanii wa muziki, kusaidia mikakati yake ya kupata kura dhidi ya wapinzani wake.

Wafuasi wake wanasema kuwa, anaonesha kuwa ni mtu wa kufikiwa kwa urahisi. 

clouds stream