Wednesday 22 February 2017

Ridhiwani Asema Haya Kuhusu Kuchunguzwa Madawa Ya Kulevya

Ridhiwani Kikwete
Ridhiwani Kikwete
img-20161130-wa0008

Sakata la madawa ya kulevya linaendelea kuchukua sura mpya siku hadi siku na sasa Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete ameibuka na kueleza ya moyoni mwake baada ya hapo jana gazeti moja la kila siku kuwa na kichwa cha habari ‘Ridhiwani achunguzwa’.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram mbunge huyo ameandika yafuatayo;

“Ni jambo jema na la faraja kubwa kwangu kama uchunguzi unafanywa, ni ukombozi kwangu, ukweli utajulikana kuwa ni uvumi tu usiokuwa na chembe ya ukweli”
“Ni maneno ya watu wasionitakia mema, sina la kuficha…sifanyi biashara hiyo haramu na wala sijawahi kufikiria kufanya…..ni bora kufa masikini kuliko kutafuta utajiri kwa njia hiyo.”
rrrrr

clouds stream