Sunday 5 February 2017

Mihadarati: Polisi 12 wasimamishwa kazi Tanzania

Inspekta jenerali wa polisi nchini Tanzania Ernest Mangu

Inspekta jenerali wa polisi nchini Tanzania Ernest Mangu
img-20161130-wa0008

Kikosi cha polisi nchini Tanzania kimewasimamisha kazi kwa muda maafisa 12 wa polisi ambao ni miongoni mwa wale waliotajwa na kamishna wa polisi wa jimbo la Dar es Salaam bw Paul Makonda miongoni mwa watu wanaoshirikishwa na ulanguzi wa mihadatari .

Pia amesema kuwa uchunguzi unaendelea dhidi ya idadi kubwa ya wasanii ambao pia walitajwa na Makonda na kuripoti katika vituo vya polisi ili kuhojiwa.

Kulingana na Gazeti la The Citizen nchini humo Inspekkta Jenerali Ernest Mangu amesema kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya maafisa hao 12 uchunguzi utakapokamilika.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Dar es Salaam Simon Sirro amesema operesheni ya kuwakamata watu hao ilianza tangu jana ambapo watu watano walitiwa korokoroni na kufikisha idadi ya watu waliokamatwa hadi leo kufikia 17.

clouds stream