Thursday 9 February 2017

Mkalimani Feki Aliyepotosha Maneno Ya Mtalii Atiwa Mbaroni


muongozzzzzzzzzzzimg-20161130-wa0008

Jeshi la Polisi limemtia mbaroni Muongoza watalii (Tour Guide) anayeonekana katika kipande cha picha ya video akipotosha tafsiri ya matamshi ya Mtalii aliyekuwa amemaliza kutembelea Mamlaka ya Bonde la Ngorongoro (NCAA).

Katika video hiyo ambayo imesambaa sana katika mitandao ya kijamii hasa WhatsApp, inamuonesha mtalii huyo ambaye jina lake halijafahamika maramoja akisema katika lugha ya kigeni (kingereza)kuwa safari yake nchini Tanzania imekuwa nzuri na kufurahia safari yake huku akikutana na watanzania waliokuwa na ukarimu na upendo kwake.

Muongozaji huyo anaonekana akitafsiri maneno ya mtalii huyo na kupotosha na kuanza kusema vitu ambavyo havikusemwa na mtalii huyo kama anawashangaa watanzania wakilalamika njaa wakati wana maua, hivyo wapike maua wale na kumtaja Rais

 Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe amesema kuwa ameagiza kukamatwa kwa mkalimani huyo feki mara tu baada ya kuona video hiyo.

“Tayari nilitoa maagizo mtu huyo atafutwe na akamatwe mara moja na kwa taarifa nilizopewa leo ni kuwa mtu huyo ameshakamatwa kwenye lango la geti la Nabi Serengeti na yupo rumande huko Mugumu,” amesema. 

clouds stream