Tuesday 7 February 2017

Madawa Ya Kulevya Yamuibua Mrema, Asema Haya

Mwenyekiti wa Bodi ya Parole Dkt. Augustine Mrema akizungumza wakati wa kukabidhiwa ripoti ya Parole. Pembeni ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini ambaye pia ni Katibu wa bodi ya Parole John Casmir Minja.
Mwenyekiti wa Bodi ya Parole Dkt. Augustine Mrema (kulia).

img-20161130-wa0008Mwenyekiti wa Taifa wa Bodi ya Parole, Augustino Lyatonga Mrema ameibuka na kusema kuwa vita ya dawa za kulevya inawezekana kumalizika kama watawatumia watumiaji na wauzaji wadogo wadogo kuwapata wale wauzaji wakubwa ambao ndiyo tatizo zaidi katika jamii.

“Vita hivi vitawezekana kumalizika kama tutatumia hawa wadogo wenye kete mbilimbili, na siyo kuwapeleka magerezani, wamenionesha na njia wanazotumia kuwapa dawa waathirika waliopo magerezani, tusitumie nguvu nyingi kuwakamata hawa dagaa wadogo wadogo, bali tuwatumie hawa tupate chain nzima, kwa njia hiyo tutapeleka watu wanaostahili magerezani,” amesema Augustino Mrema.

Ameongeza kuwa wapo baadhi ya polisi wanagawa na kusambaza dawa za kulevya pia wanawasaidia baadhi ya waathirika wa dawa hizo waliopo magerezani kuzipata.

Mbali na hilo Augustino Lywatonga Mrema amesema kama polisi walikuwa wanasambaza na kugawa madawa ya kulevya hivyo basi wao ndiyo walikuwa wakiendesha hivyo vijiwe na kuwajua wahusika wa madawa ya kulevya.

“Sasa kama polisi ndiyo anasambaza na kugawa madawa kwa hiyo vijiwe vile vilikuwa vinaendeshwa na wao, hivyo wanawajua wanaogawa, na wanaotumia sasa huu mtandao ukikamatwa hii nchi itapona,” ameongeza Mrema.

clouds stream