Urais 2015: CUF yamteua Prof. Lipumba kugombea urais
Dares salaam, Hatimaye Chama cha wananchi CUF leo kimetangaza
kupeleka jina la Mwenyekiti wa Chama cha CUF Prof. Ibrahim Lipumba
katika umoja wa katiba ya wananchi UKAWA. Jina hilo litaunganishwa na
majina ya wanachama wengine katika umoja wa katiba ya wananchi
achaguliwe kuiwakilisha Ukawa ambapo atapambana na kada kutoka chama
tawala cha Mapinduzi (CCM).
Kwa mujibu wa Naibu mkurugenzi wa uchaguzi wa chama cha wananchi CUF Bwana Shaweji Mketo amesema kuwa kwa mujibu wa makubaliano na vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi kila chama kitateua mgombea katika nafasi zote na kisha kushindanisha ili kupata mgombea moja atakayeungwa mkono na vyama vyote.
Ameongeza kuwa katika nafasi ya viti vya udiwani na ubunge kwa wanaotaka kugombea fomu zitaanza kutolewa kuanzia machi 1 hadi 10 kupitia makatibu wa matawi na katika nafasi ya ubunge wagombea watatakiwa kuchukua fomu kwa makatibu kata na kuzirudisha kwa makatibu wa wilaya.
Katika hatua nyingine amesisitiza kuwa aprili 17 hadi 19 kurugenzi ya uchaguzi inatarajia kukaa na kufanya mchujo kwa wagombea ubunge
Kwa mujibu wa Naibu mkurugenzi wa uchaguzi wa chama cha wananchi CUF Bwana Shaweji Mketo amesema kuwa kwa mujibu wa makubaliano na vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi kila chama kitateua mgombea katika nafasi zote na kisha kushindanisha ili kupata mgombea moja atakayeungwa mkono na vyama vyote.
Ameongeza kuwa katika nafasi ya viti vya udiwani na ubunge kwa wanaotaka kugombea fomu zitaanza kutolewa kuanzia machi 1 hadi 10 kupitia makatibu wa matawi na katika nafasi ya ubunge wagombea watatakiwa kuchukua fomu kwa makatibu kata na kuzirudisha kwa makatibu wa wilaya.
Katika hatua nyingine amesisitiza kuwa aprili 17 hadi 19 kurugenzi ya uchaguzi inatarajia kukaa na kufanya mchujo kwa wagombea ubunge