Tuesday 24 October 2017

MUGABE ‘ATUMBULIWA’ SIKU CHACHE BAADA YA KUTEULIWA BALOZI



Rais Robert Mugabe.



Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), ametengua uteuzi wa Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ambaye aliteuliwa kuwa
Balozi mwema wa Shirika hilo siku chache zilizopita.

Imedaiwa kuwa sababu za kutengua uteuzi huo ni kutokana na malalamiko mengi kutoka kwa watu.
Tangu taarifa za uteuzi wake zisambae, viongozi wengi kutoka pande mbalimbali duniani walionekana kutokukubaliana na uteuzi
huo hivyo kukosoa uamuzi wa shirika hilo.

Mugabe ambaye ni mmoja wa marais waliokaa madarakani kwa muda mrefu barani Afrika amekuwa akishutumiwa kwa kukandamiza demokrasia nchini Zimbabwe ikiwa ni pamoja na kufanya mbinu ili kuweza kusalia madarakani hadi pale
atakapochoka mwenyewe.

clouds stream