Monday 16 October 2017

Takriban watu 230 wauawa kwenye milipuko Mogadishu

Takriban watu 230 wauawa kwenye milipuko Mogadishu

Takriban watu 230 wauawa kwenye milipuko Mogadishu


Sasa imebainika kuwa idadi ya watu waliouawa katika mashambulio mawili ya mabomu mjini Mogadishu, Somalia, imepanda na kuwa zaidi ya 230.

Mamia ya watu wengine wanaripotiwa kujeruhiwa.

Hilo ndilo shambulizi baya zaid kuwahi kutokea nchini Somalia tangu kundi la al-Shabab lianzishe harakati zake mwaka 2007.

Haijulikani nani alihusika, lakini kwa idadi ya maafa, hayo yalikuwa kati ya mashambulio makubwa kabisa nchini Somalia, tangu kundi la wapiganaji wa Kiislamu, al-Shabab, kuanza mapigano yao mwaka 2007.


Takriban watu 230 wauawa kwenye milipuko Mogadishu


Katika shambulio la kwanza, bomu lilokuwa kwenye lori, lililipuka kwenye njia panda, iitwayo Kilomita-5, ambapo kuna ofiisi za serikali, mahoteli na maduka, vyote viliporomoka katika mlipuko huo.


Saa mbili baadaye, bomu jengine lilikalipuka katika mtaa wa Medina.


Mkurugenzi wa Hospitali ya Madina, Mohamed Yusuf Hassan, anasema, alishtushwa na ukubwa shambulio hilo.

Takriban watu 230 wauawa kwenye milipuko Mogadishu

clouds stream