Wednesday 12 July 2017

Jeshi la China laelekea kuweka kambi ya kwanza ya kigeni Djibouti



Picture of Chinese naval personnel in Djibouti in 2015

Wanajeshi wanamaji wa China
IMG-20170426-WA0006

Meli zinazowasafirisha wanajeshi wa China zinaelekea nchini Djibouti kuweka kambi ya jeshi ya China ambayo ndiyo ya kwanza ya kigeni.

China inasema kuwa kambi hiyo itatumiwa kwa huduma za kulida amani na za kibinadamu barani Afrika na magharibi mwa Asia.

Pia itatumiwa kwa ushikiano wa kijeshi, mazoezi ya kijeshi na huduma za uokoaji.

China imewekezaa katika nchi za kiafrika na pia imeboresha kwa haraka jeshi lake miaka ya hivi karibuni.

Map showing Djibouti in Africa
Djibouti

Shirika la habari ya Xinhua lilisema kuwa meli hizo ziliondoka bandari ya Zhanjiang katika mkoa wa kusini wa Guangdong siku ya Jumanne.

Halikutaja idadi ya wanajeshi au meli zilizoplelekwa Djibouti au ni lini kituo hicho kitaanza kutangaza huduma zake.

Xinhua linasema kuwa kituoa hicho cha Djibouti kinabuniwa kufuatia mazungumzo kati ya nchi hizo mbili.

Kituo hicho kinaonekana kama hatua ya China ya kuwa na usemi wa kijeshi eneo hilo.

Chinese employees of the Addis Ababa / Djibouti train line stand at the Feri train station in Addis Ababa on 24 September 2016.
China imejenga reli inayoungasha Djibouti na Addis Ababa

clouds stream