Wednesday 12 July 2017

Marekani na Qatar waafikiana kuukabili ugaidi duniani

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Rex Tillerson (kushoto) akiwa na waziri wa mambo ya nje wa Qatar Sheikh Mohammed bin Abdulrahman al-Thani mjini Doha

IMG-20170426-WA0006

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Rex Tillerson (kushoto) akiwa na waziri wa mambo ya nje wa Qatar Sheikh Mohammed bin Abdulrahman al-Thani mjini Doha

Marekani na Qatar wamefikia makubaliano ya jitihada za kukabiliana na kudhamini ugaidi.

Makubaliano hayo yametiwa saini mjini Doha na waziri wa mambo ya nje wa Marekani Rex Tillerson ambaye yuko ziarani nchini humo.

Makubaliano hayo yanafanyika wakati ambapo Qatar ipo katika mgogoro mkali na majirani zake, ikiwemo Saudi Arabia.

Wote wamekata uhusiano na Qatar baada ya kuituhumu kuunga mkono makundi ya wapiganaji wa kiislamu katika eneo la Mashariki ya Kati.

Tillerson ameisifu Qatar kuwa ni nchi inayoupinga ugaidi
Tillerson ameisifu Qatar kuwa ni nchi inayoupinga ugaidi

Wachambuzi wa mambo ya kisiasa wanasema, makubaliano hayo na Marekani, ambayo inasaidia kusuluhisha mgogoro huo, imeashiria kwamba inaiona Qatar kama mshirika mwaminifu katika mapambano dhidi ya ugaidi.

clouds stream