Monday 31 July 2017

Marekani: Muda wa mazungumzo kuhusu Korea Kaskazini umekwisha

The US B-1 bombers were joined by South Korean and Japanese planes

IMG-20170426-WA0006

Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe anasema yeye pamoja na rais wa Marekani Donald Trump wamekubaliana kuwa upo umuhimu wa kupambana na Korea ya Kaskazini katika mipango yake ya majaribio ya makombora.

Abe amewaambia waandishi wa habari kuwa anashukuru kujitolea kwa Rais Trump katika suala la Korea ya Kaskazini.

Mapema Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Nikki Haley alisema muda wa mazungumzo umemalizika.

Nikki Haley
Mapema Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Nikki Haley alisema muda wa mazungumzo umemalizika.

Haley amesema hakuna sababu ya kuwa na kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa iwapo hakutakuwa na matokeo, yatakayoipa mbinyo Korea Kaskazini na China ni lazima iamue kama itaamua kuchukua hatua hii muhimu.

Hatua hiyo imekuja baada ya Korea kaskazini kufanya jaribio lingine la makombora yake siku ya Ijumaa.

A Terminal High Altitude Area Defense (THAAD) interceptor is launched during a successful test, 29 July 2017
Marekani imesema kuwa mtambo wake wa kuangusha makombora wa Thaad umefanikiwa
Map showing estimates of North Korean missile ranges
Mchoro wa kuonyesha uwezo wa makombora ya Korea Kaskazini
Thaad missile defence system graphic
Jingi mfumo wa Thaad unafanya kazi

Thaad system launcher
Thaad

clouds stream