Monday 24 July 2017

Vitisho vya China vyasababisha Vietnam kusitisha uchimbaji wa gesi baharini

This picture taken by Vietnam News Agency and released on June 14, 2011 shows Vietnamese sailors patrolling on Phan Vinh Island in the Spratly archipelago

Vitisho vya China vyasababisha Vietnam kusitisha uchimbaji wa gesi

Vietnam imesitisha shughuli ya uchimbaji gesi katika eneo linalozozaniwa kusini mwa bahari ya China, kufuatia vitisho vikali kutoka China.

Taarifa zinaiambia BBC kuwa kampuni iliyokuwa ikiendesha uchimbaji huo iliamrishwa kuondoka eneo hilo.

Inajiri siku chache baada ya kampuni ya Respol kusema kuwa imegundua gesi nyingi.

Ripoti zinasema kuwa wakurugenzi wa Respol waliambiwa wiki iliyopita na serikali wa Viertman kuwa China ilikuwa imetisha kushambulia vituo vyake katika visiwa vya Spratly ikiwa uchimbaji huo haungesitishwa.

South China Sea
Vitisho vya China vyasababisha Vietnam kusitisha uchimbaji wa gesi

China inadai kuwa karibu eneo lote la kusini mwa bahari ya China ni lake, visiwa ambavyo pia vinavyodaiwa na mataifa mengine.

Vietnam inaliita eneo hilo Block 136-03 na imeipa zabuni kampuni inayoitwa Talisman-Vietnam.

China nayo inaliita eneo hilo Wanan Bei-21 ikiwa imetoa kandarasi kwa kampuni tofauti.

This picture taken on 14 May shows a Chinese coast guard ship (back) sailing next to a Vietnamese coast guard vessel (front) near China's oil drilling rig in disputed waters in the South China Sea.
Vitisho vya China vyasababisha Vietnam kusitisha uchimbaji wa gesi

clouds stream