Sunday 16 July 2017

KAMPENI MBIO ZA URAIS NCHINI RWANDA ZAANZA RASMI

19990259_1608504162501576_4840364669151194404_n
IMG-20170426-WA0006

Wakati nchi ya Kenya ikijiandaa kufanya Uchaguzi Mkuu Agosti 8, mwaka huu, shughuli za kampeni za uchaguzi wa Rais nchini Rwanda zimeanza rasmi ambapo wagombea wa kiti cha urais ni watatu, Rais Paul Kagame anayewania muhula wa tatu baada ya Katiba ya nchi hiyo kubadilishwa.

Kagame anapambana na Frank Habineza wa Chama cha Green na Philippe Mpayimana ambaye ni Mgombea wa Kujitegemea.

Mgombea wa Urais kwa tiketi ya Chama Tawala RPF, Rais Paul Kagame alianzia kampeni kusini mwa Rwanda, Mjini Ruhango na mgombea wa kujitegemea Philippe Mpayimana alianzia kampeni kusini mashariki mwa nchi hiyo.19990329_1608504242501568_2989829514862107736_n20031628_1608504092501583_4418943849987591928_n

clouds stream