Saturday 22 October 2016

Bodaboda Iliyotelekezwa Yazua Maajabu, Yaogopwa Na Polisi,Raia

pikipiki
V 2
Boda boda yente maajabu ikiwa imepigwa vumbi kwa muda wa mwaka mmoja bila kuguswa na mtu yeyote.

Pikipiki aina ya Fekoni yenye namba za usajili T684 CJZ imeonekana kuwa ya maajabu kufuatia kutelekezwa na kuogopwa na watu katika kituo cha Waendesha Bodaboda cha Maganga Veterinary jijini Dar es salaam.

Wakizungumzia bodaboda hiyo waendesha Bodaboda wanaopaki katika kituo hicho wameiambia HivisasaBlog kuwa Bodaboda hiyo imeshakaa hapo kituoni zaidi ya mwaka mmoja sasa, haijulikani nani hasa mmiliki wa Bodaboda hiyo.

Bodaboda hiyo inadaiwa kuwa licha kukaa mwaka mmoja bila kuguswa, ukikaribia inajiwasha,hivyo Jeshi la Polisi na Raia kushindwa kuiondoa katika eneo ilipopaki.

“Mwandishi hii Bodaboda sio ya kawaida,yaani ipo hapa zaidi ya mwaka na hakuna wa kuigusa kutokana na kama ina mauza mauza vile maana ukiikaribia inajiwasha yenyewe wakati pale ilipo haina funguo na Mwenye funguo hajulikani yuko wapi”.Alisema mmoja wa wendesha Bodaboda.

clouds stream