Wednesday 26 October 2016

Serikali Yapiga Marufuku Michakato Ya Kubadili Umiliki Simba Na Yanga

mabasi1V 2

Serikali kupitia Baraza la Michezo Tanzania (BMT) imetoa agizo la kusitishwa kwa michakato ya kubadilisha umiliki wa timu za Simba na Yanga.

Inataka klabu hizo zibaki kwa wanachama kama ilivyo sasa na kwa muda mrefu tangu kuanza kwa vilabu hivyo.

Hivi karibuni kumekuwa na malumbano kuhusu umiliki wa vilabu hivyo baada ya wafanyabiashara wawili wakubwa Yusuph Manji (Yanga) na Mohamed Dewji ‘MO’ (Simba) ambapo Manji anataka kukodishiwa klabu ya Yanga kwa muda wa miaka kumi huku MO akitaka kuwa na hisa zaidi ya 51 katika klabu hiyo.

clouds stream