Saturday 1 October 2016

Mr Na Miss HIV Wapatikana

Tarehe October 2, 2016
ctqlmkexgaax6tsV 1
Mashindano ya kumtafuta kijana mtanashati (Mr) na Mrembo (Miss) waishio na virusi vya ukimwi (VVU) yamefanyika nchini Uganda na washindi kupatikana.
Nchini Uganda warembo wanaoishi na virusi vya ukimwi {VVU} wanashiriki mashindano ya kumpata malkia wa taji la warembo hao huku lengo likiwa ni kuondoa unyanyapaa dhidi ya watu wenye VVU.
Katika hatua za awali lilipotangazwa shindano hilo inasemekana takribani watu 150 walijitokeza wakitaka kushiriki katika shindano hilo.
Mashindano hayo pia yalihusisha watu wenye vipaji mbalimbali sio uzuri peke yake.
Inasemekana Uganda ni kati ya nchi zenye watu wengi wanaoishi na virusi vya UKIMWI, kwa takwimu za hivi karibuni zinasema mtu mmoja kati ya 14 ana maambukizi ya UKIMWI.ctqlmkexgaax6ts

clouds stream