Friday 22 May 2015

Marekani yaomba radhi vifo vya watoto Syria

Marekani yaomba radhi vifo vya watoto Syria


Marekani yakiri kuua raia nchini Syria.
Marekani yakiri kuua raia nchini Syria.
Marekani imekiri, kwa mara ya kwanza kuhusika na mapigano ya anga dhidi ya kikosi cha kiislamu yaliyopelekea baadhi ya raia kuuawa. Katika mkutano wa dharula Pentagon Mkuu wa kikosi Luteni Jenerali James Terry ,aliomba radhi kwa mauaji ambayo yalitokea bila kukusudia na kuua watoto wawili waliouawa wakati wa machafuko nchini Syria mwaka jana.
Kufuatia tukio lililotokea mjini Palmyra na Ramadi katika kipindi cha wiki limehusishwa kama kisasi . Ingawa Rais Obama alisisitiza kuwa Marekani ilikuwa si ya kupoteza vita na wapiganaji . Rais aliahidi msaada zaidi kwa vikosi vya usalama nchini Iraq na kusema Marekani itajaribu kuongeza mafunzo ya kijeshi katika maeneo ya Sunni.
Siku moja baada ya mji wa Syria wa Palmyra kuanguka , Wakazi wa eneo hilo wanasema waislamu wenye siasa kali bado wanawasaka wale wanaounga mkono serikali.
Hata hivyo wapiganaji wa Kiislamu wameripotiwa kuwa wengi zaidi ya ulinzi wa eneo la mashariki mwa Iraq, huku wakijaribu himaya yao huko.

clouds stream