Tuesday 26 May 2015

Real Madrid wafukuza kocha

Real Madrid wafukuza kocha

Tarehe May 26, 2015
_83218614_carlo_ancelotti_getty-2

Baada ya kushindwa kuifikisha Real Madrid kwenye hatua ya fainali kwenye ligi ya mabingwa barani ulaya na pia kushindwa kuchukua ligi kuu nchini Hispania imekuwa kama moja ya mambo yaliyofanya kocha wa Carlo Ancelotti kufukuzwa. Carlo Ancelotti alipofanya mahojiano na waandishi wa habari siku ya ijumaa alisema anaamini ataendelea kuifundisha timu hiyo msimu ujao huku wachezaji kama Cristiano Ronaldo na James Rodriguez wakiamini kuwa na kocha wao msimu ujao.
Maamuzi ya Real Madrid kumfukuza Carlo Ancelotti yalifanyika jana baada ya rais wa timu hiyo Florentino Perez kuonyesha wazi siku za karibuni kwa maneno yake kuwa kocha huyo amebakiza siku chache kwenye klau hiyo, nuamuzi huo wa Real Madrid unaongeza tetesi kwenye masikio ya mashabiki wa Real Madrid kuwa kocha atakaechukua kiti hicho ni Rafa Benitez.

clouds stream