Tuesday 9 August 2016

Magufuli Kutikisa Viwanja Vya Furahisha Mwanza.

Tarehe August 10, 2016
Rais Dkt.John Pombe Magufuli.V 1

Rais Dkt.John Pombe Magufuli. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa mara ya kwanza anatarajia kuweka historia ya kuhutubia katika Viwanja vya Furahisha jijini Mwanza tangu alipochaguliwa kuwa Rais wa Tanzania.

Kwa mujibu wa Mkuu wa mkoa wa Mwanza Bw. John Mongela amesema Rais Magufuli atawahutubia wananchi katika viwanja hivyo kesho na kuwataka wanachi kujitokeza kwa wingi katika mkutano huo mkubwa wa kisiasa.

Viwanja vya Furahisha ni moja ya viwanja vilivyojipatia umaarufu mkubwa kutokana na wanasiasa pamoja na viongozi wa serikali kuvitumia kuwakuhutubia wananchi.

clouds stream