Thursday 4 August 2016

Mahakama Yasaidia Upatikanaji Wa Kodi Ya Bilioni 2.1 Kutoka Kwa Wadaiwa Sugu.

Tarehe August 5, 2016
10792822-Blank-highway-billboard-sign-in-an-outdoor-display-showing-a-road-representing-the-concept-of-focuse-Stock-PhotoV 1

Takribani shilingi bilioni mbili na milioni 123 zimekusanywa na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kutoka kwa wadaiwa sugu wa kodi mbalimbali baada ya kufikikishwa mahakamani.

Mwanasheria wa Halmashauri hiyo, Bonaventure Mwambaja ameyasema hayo katika kikao cha Baraza la Madiwani na kudai kuwa kwa mwaka wa fedha 2014/15 jumla ya wafanyabiashara 72 walipelekwa mahakamani ambapo hadi kufikia Julai 30, mwaka huu kiasi hicho cha fedha kilikuwa kimekwishakusanywa kutoka kwa wadaiwa hao sugu.

 Amesema hadi mtu afikishwe mahakamani anakuwa ameshapatiwa hati ya madai (Demand Note) ambayo inamtaka mhusika kulipa kodi anayodaiwa ndani ya siku 14 hadi 30, na baada ya muda huo kupita basi sheria lazima ifuate mkondo wake.

Kodi hizo ni pamoja na kodi za majengo na mabango, kodi za huduma mbalimbali pamoja na kodi ya leseni za biashara.

Naye Mstahiki Meya wa Halmashauri hiyo, Charles Kuyeko ameshauri wananchi kutoa ushirikiano kwa watendaji pindi wanapowatembelea kuchukua kodi kwa kuwa ukusanyaji wa kodi huongeza pato la Taifa kwa kiasi kikubwa.

clouds stream