Monday 29 August 2016

Mbwana Samatta Afunika Ligi Za Ulaya

Tarehe August 29, 2016
mbwana-samatta_2nx5mzohoms410k2eiy1i42znV 1
Nahodha wa Taifa stars na Straika wa Ubelgiji,Mbwana Samatta,ameonekana kuuanza msimuu huu kwa nguvu na kasi kwa kuonekana kufunika baadhi ya mastaa katika ligi za Ulaya .
Mchezaji huyo Samatta aliyekuwa amejiunga na dirisha dogo msimu uliopita akitokea katika timu ya TP Mazembe ya Congo , kabla ya mechi iliyo chezwa jana Jumaapili alikuwa akionekana kuwafunika wachezaji wenzake akiwemo Wayne Rooney pamoja na Ibrahimovic wakiwa wote ni wachezaji wa Manchester United.
Pia Samatta anaongoza kwa mabao yapatayo manne ,hali ya kuwa Ibrahimovic akiwa na jumla ya mabao yapatayo matatu huku Mchezaji Rooney kuonekana akiwa hana ata bao moja .
Licha ya Mbwana Samatta kuonekana kuwa kidedea kati ya wachezaji hao ,ameonekana kupigwa bao na mchezaji anaye waniwa na kocha wa Arsenal,Arsene Wenger,Alexandre Lacazette anayekipiga Olympique Lyon ya Ufaransa mwenye mabao sita.
Huu ni mwanzo mzuri wa mchezaji Samatta kwani kuonekana kwake kuwa bigwa dhidi ya wachezaji wakogwe ni moja ya hatua kwa upande wake .
Pia Mbwana Samatta ameonekana akifunga mabao yake kwa kiwango cha juu tofauti na wachezaji wengine wa Tanzania kwani yeye huonekana akitumia ufundi wake kama Mastraika wakubwa.

clouds stream