Monday 15 August 2016

Sababu Ya Mgosi Kustaafu Mapema Hii Hapa.

Tarehe August 15, 2016
Mussa Hasan Mgosi akiwa na mwanae mara baada ya kuwaaga rasmi mashabiki wa Simba FcV 1
Mussa Hasan Mgosi akiwa na mwanae mara baada ya kuwaaga rasmi mashabiki wa Simba Fc.

Nahodha wa Simba, Mussa Hassan Mgosi aliyetangaza kustaafu amesema kuwa sababu kubwa iliyomfanya astaafu mapema ni kutokupenda hadi mashabiki wa mzomee uwanjani.

Amesema aliamua kustaafu akiwa anaheshimika, anahitajika na ndiyo maana amefurahi kuondoka katika kipindi hiki.

“Nimeondoka katika kipindi ninahitajika, ninafurahi kwa kuwa bado nitaendelea kubaki ndani ya kikosi cha Simba na kutoa msaada wangu,” alisema.

“Bora kuondoka mapema wakati unahitajika kuliko kusubiri kipindi cha malumbano, au mashabikikuanza kulalamikia.

“Niwashukuru sana Wanasimba wote kwa ushirikiano wao, naomba waiunge mkono timu yao katika kipindi kigumu au kile cha furaha,” alisisitiza.

Mgosi sasa anachukua nafasi ya Meneja wa kikosi cha Simba na ataendelea kushirikiana na wachezaji.

Mgosi alipata nafasi ya kuichezea timu hiyo mara ya mwisho katika kikosi hicho.

clouds stream