Friday 12 August 2016

Sikia Kauli Ya Kifukwe Kuhusu Manji,Pia Jua Kinachosubiriwa Sasa.

Tarehe August 12, 2016
Yusuf Manji akifungua mkutano pamoja na kuwasilisha ajenda za mkutanoV 1
Yusuf Manji akifungua mkutano pamoja na kuwasilisha ajenda za mkutano .

Wazo la mfanyabiashara Yusuf Manji kutaka kukodishiwa klabu ya Yanga kwa miaka kumi limeendelea kushika vichwa vya habari katika magazeti na baadhi ya wadau wa michezo.

Moja ya watu waliongelea suala hilo ni Mjumbe wa baraza la wadhamini wa timu hiyo Francis Mponjoli Kifukwe ambaye amesisitiza kusubiri ombi hilo la Manji katika maandishi.

“Japo wanachama wamekubali 100% lakini tunasubiri mapendekezo yake rasmi katika maandishi, ili sisi (Baraza la Wadhamini) tuanze kuyafanyia kazi,tuone klabu klabu yetu itanufaika vipi katika muda huo wa miaka 10 chini yake”alisema Francis Mponjoli Kifukwe .

clouds stream