Thursday 26 March 2015

Rais Kikwete ateua wabunge wawili wapya

Rais Kikwete ateua wabunge wawili wapya

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, amewateua wabunge wawili wapya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Walioteuliwa ni Dkt. Grace Khwaya Puja na Bwana Innocent Sebba ambapo Rais amefanya uteuzi huu kwa mamlaka aliyopewa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 66 (I) (e) ambapo amepewa mamlaka ya kuteua wabunge wasiozidi 10.
Uteuzi huu umekamilisha idadi ya wabunge ambao Mheshimiwa Rais amepewa kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo Kikatiba ambao waliokwishateuliwa ni Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa, Mhe. Profesa Sospeter Muhongo, Mhe. Dkt. Asha Rose Migiro, Mhe. Janet Zebedayo Mbene, Mhe. Saada Salum Mkuya, Mhe. Zakhia Hamdani Meghji, Mhe. Shamsi Vuai Nahodha, na Mhe. James Mbatia.

clouds stream