Wednesday 11 March 2015

Majeshi ya Iraq yaukomboa mji uliotekwa na Islamic State

Majeshi ya Iraq yaukomboa mji uliotekwa na Islamic State


Maofisa wa serikali nchini Iraqi wamesema kwamba majeshi ya serikali yanayoungwa mkono na majeshia ya Shia yamefanikiwa kuyakomboa baadhi ya maeneo ya mji wa Tikrit kutoka katika himaya ya wanamgambo wa dola ya kiislam Islamic State .
Majeshi hayo ya serikali yalianza mapigano ya kuikomboa Tikrit kwa kuukomboa mji wa Alam ulioko Kaskazini nje kidogo ya mji huo wa Tikrit. Ingawa wakazi wa eneo hilo la wanadai kuwa wanamgambo wa Islamic State wametega mabomu maeneo mengi ya mji huo ili kuchelewesha majeshi ya serikali kuukomboa mji huo.
Mashambulizi katika mji wa Tikrit unaofanywa na majeshi ya serikali ni makubwa kwa sasa katika operesheni dhidi ya wanamgambo hao.
Majeshi ya Iraq yanaendesha operesheni hiyo kwa msaada wa ushauri wa kijeshi kutoka Iran bila msaada wa Marekani katika mashambulizi ya angani.
Kwa furaha raia wamekuwa wametoka nje ya nyumba zao kuwasalimia wanajeshi wa serikali Iraq na wapiganaji wa Shia.

clouds stream