Tuesday 31 March 2015

Mwendesha mashtaka kesi ya ugaidi auawa kwa risasi

Mwendesha mashtaka kesi ya ugaidi auawa kwa risasi


kageziss-600x360
Mkurugenzi Msaidizi wa Mashtaka ambaye alikuwa akiongoza upande wa mashtaka katika kesi ya tukio la ugaidi la Jijini Kampala, lililotokea Julai 2010 nchini Uganda ameuawa jana jioni kwa kupigwa risasi.
Kwa  mujibu wa polisi nchini humo wamesema Joan Kagezi, aliuawa saa mbili usiku na watu wenye silaha waliokuwa wakiendesha pikipiki katika eneo la Kiwatule, lililopo nje kidogo ya Jiji la Kampala, wakati akirejea nyumbani.
Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Upelelezi, Grace Akullo, amethibitisha tukio hilo ambapo amesema mwili wa Kagezi, umehifadhiwa kwenye hospitali ya Mulago, na uchunguzi wa mauaji yake unaendelea.

clouds stream