Wednesday 17 February 2016

Cavan Aimaliza Chelsea Akitokea Benchi,PSG -2 Vs Chelsea -1

Cavan Aimaliza Chelsea Akitokea Benchi,PSG -2 Vs Chelsea -1

Tarehe February 17, 2016
Edinson Cavan
Edinson Cavan
Chelsea imeshindwa kuwika jijini Paris walipokwenda kuivaa Paris Saint Germain kwa kukubali kufungwa magoli mawili kwa moja katikamchezo wao wa klabu bingwa ya dunia uliomalizika hivi punde.
Zlatan Ibrahimovic aliipatia PSG goli la kwanza baada ya kupiga mkwaju wa adhabu dakika ya 39 baada ya Obi Mikel kufanya madhambi.
Dakika ya 45 Obi Mikel aliipatia Chelsea goli la kusawazisha na kufanya timu hizo ziende mapumziko zikiwa zimefungana 1-1.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku PSG wakimtumia sana Di Maria kumlisha mipira Ibrahimovic ,Edinson Cavan aliingia kama mchezaji wa akiba na kuifungia PSG goli la ushindi dakika ya 78.
Na mpaka mpira unamalizika PSG walikuwa mbele kwa magoli 2-1.

clouds stream