Saturday 20 February 2016

Museveni Ashinda Urais Uganda

Museveni Ashinda Urais Uganda

Tarehe February 20, 2016
Rais Yoweri Museveni wa Uganda.
Rais Yoweri Museveni wa Uganda.
Tume ya Uchaguzi nchini Uganda imemtangaza Rais Yoweri Museveni kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika Alhamisi.
Rais Museveni alipata kura 5,617,503 sawa na asilimia 60.75 ya kura zilizohesabiwa kwa mujibu wa mwenyekiti wa tume hiyo Dkt Badru Kiggundu.
Mpinzani wake mkuu Dkt Kizza Besigye alipata kura 3,270,290 ambazo ni sawa na asilimia 35.37%.
Museveni ametangazwa mshindi licha ya kwamba kuna vituo ambavyo bado matokeo hayajatangazwa.
Kwa mujibu wa Dkt Kiggundu amesema matokeo ya vituo hivyo hayawezi kubadilisha mambo.

clouds stream