Sunday 14 February 2016

Trump Ataka Wazungu Waitawale Tena Afrika, Je Unakubaliana Naye

Trump Ataka Wazungu Waitawale Tena Afrika, Je Unakubaliana Naye

Tarehe February 14, 2016
Donald Trump
Donald Trump
Mfanyabiashara wa kimarekani, na Mgombea Urais,  Donald Trump amesema Afrika inahitajika kutawaliwa tena. Mara hii ameonyesha ghadhabu zake kwa viongozi wa Afrika ambao kwa mujibu wa Trump, wameshindwa kuongoza na kuwabakisha watu wao kwenye hali mbaya zaidi.
Akiongea jana mjini Nebraska, Trump amesema waafrika ni watumwa wanaoishi kitumwa kwenye ardhi yao wenyewe na bado wanajiita wako huru.
Trump alikuwa akijibu swali la mwandishi wa habari kutoka Afrika ya kusini kama anafikiri viongozi wa kiafrika walikuwa sawa kutaka kutoka mahakama ya kimataifa ya uhalifu ‘The Hague’.
“Ni aibu kwa viongozi wa Afrika kutaka kutoka ICC. Kwa mtazamo wangu, viongozi hawa wa kiafrika wanahitaji uhuru wa kuwakandamiza watu wao maskini bila mtu yeyote kuwauliza maswali.
Nafikiri hamna njia fupi kuelekea kwenye ukomavu na kwa mtazamo wangu, Afrika inatakiwa kutawaliwa tena kwa sababu waafrika bado wapo kwenye ukoloni.
Angalia jinsi hawa viongozi wa kiafrika wanavyobadili katiba kwa maslahi yao ili waishi marais. Wote wana tamaa na hawawajali watu wa kawaida” Alisema Trump.

clouds stream