Saturday 27 February 2016

Uchaguzi Wa Meya Dar Wakumbwa Na Vurugu

Uchaguzi Wa Meya Dar Wakumbwa Na Vurugu

Tarehe February 27, 2016
Baadhi ya Polisi katika Ukumbi huo wa uchaguzi wa Meya.
Baadhi ya Polisi katika Ukumbi huo wa uchaguzi wa Meya.
Uchaguzi wa Meya wa jiji la Dar es salaam umeahirishwa tena leo kufuatia kuibuka kwa vurugu kubwa wakati tangazo la kuahirishwa uchaguzi huo lilipotolewa.
Chanzo  cha vurugu hizo  Katika ukumbi huo wa Karimjee kinadaiwa kuwa ni mkurugenzi wa Jiji kutangaza kuahirisha uchaguzi huo kwa madai ya uchaguzi  kuwekewa pingamizi na CCM mahakamani.
Suala hilo limewakasirisha madiwani wa UKAWA ambao walidai kuwa hawajapata barua ya pingamizi hilo, hivyo wakataka waruhusiwe kufanya uchaguzi peke yao kwa kuwa akidi ya madiwani kufanya uchaguzi ilikuwa imetimia.
Wakati UKAWA  wakijiiandaa kufanya uchaguzi huo  wenyewe, Polisi zaidi ya 15 walivamia ukumbi huo na kuwataka madiwan hao waondoke ukumbini, jambo lilowachukiza tena na kuibua vurugu ndani ya ukumbi.
Uchaguzi huo leo umeahirishwa kwa mara ya nne huku kukiwa na dalili ya figisu figisu inayoedelea kuwamisha uchaguzi huo.
Jeshi la Polisi likituliza vurugu katika uchaguzi wa Meya wa Dar.
Jeshi la Polisi likituliza vurugu katika uchaguzi wa Meya wa Dar.
Mbunge wa Kibamba, John Mnyika akizungumza na Waandishi wa habari katika ukumbi wa Karimjee jijini Dares salaam leo.
Mbunge wa Kibamba, John Mnyika akizungumza na Waandishi wa habari katika ukumbi wa Karimjee jijini Dares salaam leo.

clouds stream