Thursday 17 March 2016

Bayern Wachomokea Kwenye Extra Time Washinda 4-2 Dhidi Ya Juventus

Bayern Wachomokea Kwenye Extra Time Washinda 4-2 Dhidi Ya Juventus

Tarehe March 17, 2016
Thomas Muellar
Thomas Muellar
Baryen wametinga robo fainali ya mabingwa ulaya baada ya kukomaa na kuitandika miamba ya soka italia Juventus magoli manne kwa mawili katika mchezo uliomalizika hivi punde.
mchezo wa awali timu hizo zilitoka sare ya magoli mawili kwa mawili hivyo ushindi wa leo Bayern anakuwa na jumla ya magoli 6-4
Juventus walianza kuichapa Bayern wakimtumia Pogba dakika ya 5 na Juan Cuadrado dakika ya 28 magoli yalidumu hadi mapuziko lakini hali ilibadilika dakika ya 73 ambapo Robert Lewandowski alipatia Bayer goli la kusawazisha na  dakika ya 90 Mjerumani Thomas Muellar akaipeleka Juventus katika muda wa ziada.
Dakika 30 za nyongeza Bayern walionekana kucheza kwa kujiamini na dakika ya 108 Thiago Alcantara alitingisha nyavu na kuwaachaJuventus wakiduwaha lakini matumaini ya Juventus yalimalizwa na Kingsley Coman dakika ya 10 baada ya kuambaa na mpira huku mabeki wa Juventusi wakimshangaa na kumruhusu kupiga mkwaju uliomshonda kipa wa Juve.

clouds stream