Monday 14 March 2016

Samatta Kafanya Kweli Genk,Yaitungua Oostende 4-1

Samatta Kafanya Kweli Genk,Yaitungua Oostende 4-1

Tarehe March 14, 2016
Mbwana Samatta
Mbwana Samatta
Mbwana Ally Samatta anayekipiga huko Genk ya Ubelgiji  ameifungia bao ikishinda 4-1 dhidi ya KV Oostende katika mchezo wa Ligi Kuu ya Ubelgiji, maarufu kama Pro League usiku huu Uwanja wa Cristal Arena mjini Genk.
Samatta aliyeanza kwa mara ya kwanza leo tangu asajiliwe Genk Januari kutoka TP Mazembe ya DRC, alifunga bao hilo dakika ya 24 kwa kichwa akiunganisha krosi ya mshambuliaji wa Jamaica, Leon Bailey.

clouds stream